1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HRW lataka uchunguzi wa mauaji baada ya mapinduzi, Kongo

27 Mei 2024

Shirika la kimataifa la haki za binadamu la Human Rights Watch limeelezea hofu yake juu ya "madai ya mauaji ya kiholela" yaliyofanyika baada ya jaribio la mapinduzi lililotibuliwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Human Rights Watch |
Shirika la kimataifa la haki za binaadamu la Human Rights Watc laiomba Kongo kuchunguza mauaji yaliyofanyika baada ya mapinduzi yaliyoshindwaPicha: John MacDougall/AFP/Getty Images

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeelezea hofu yake leo juu ya "madai ya mauaji ya kiholela" yaliyofanyika baada ya jaribio la mapinduzi lililotibuliwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Shirika hilo lililo na makao yake mjini New York, Marekani, sasa limetoa wito kwa serikali ya nchi hiyo kufanya uchunguzi kuhusiana na madai hayo.

Human Rights Watch linasema limepata mkanda wa video uliochukuliwa na majeshi ya Kongo unaoonesha watu wanaodhaniwa kuhusika katika jaribio hilo la mapinduzi wakifyatuliwa risasi karibu na makao makuu ya rais.

Kulingana na msemaji wa jeshi Jenerali Sylvain Ekenge, karibu watu 40 walikamatwa huku wengine 4 waliuwawa. Ekenge alisema kwamba njama hiyo iliongozwa na Christian Malanga, raia wa Kongo mzaliwa wa Marekani, ambaye ni mmoja wa waliouwawa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW