Kura zahesabiwa Brazzaville, N’Guesso atarajiwa kushinda
16 Machi 2026
Matangazo
Rais anaetetea kiti chake Denis Sassou N'Guesso aliyeiongoza nchi hiyo kwa muda mrefu, anawania awamu ya tano. Matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa ndani ya wiki mbili.
Sio watu wengi waliojitokeza kupiga kura, kwa kuwa raia wengi walisema hawaamini uchaguzo huo utaleta mabadiliko ya uongozi kutoka kwa Sassou N'Guesso aliyetawala kwa miaka 42. Kabla ya uchaguzi huo upinzani ulitoa wito kwa raia kuususia.
Wagombea sita walipambana na Sassou N'Guesso mwenye miaka 82 kuwania nafasi hiyo ya juu kwenye moja ya taifa lenye hifadhi kubwa ya mafuta kusini mwa jangwa la Sahara, lakini wachambuzi tayari wamesema hakuna hata mmoja anaetarajiwa kushinda.