1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Kyiv yashambuliwa kwa droni na makombora ya Urusi

14 Novemba 2025

Jeshi la Urusi limefanya mashambulizi makubwa mapema leo kwa kutumia droni na makombora yaliyoulenga mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.

Ukraine Kyiv 2025 | Droni
Droni ya Urusi mjini Kyiv Picha: Sergei Supinsky/AFP

Maafisa wa Ukraine wamesema mashambulizi hayo yalilenga majengo mbalimbali na kusababisha milipuko na moto katika maeneo kadhaa ya mji huo.

Meya wa Kyiv, Vitali Klitschko, amethibitisha kuwa watu wawili wamejeruhiwa katika mashambulizi hayo.

Kupitia ujumbe aliouandika kwenye mtandao wa Telegram, meya huyo ameeleza kuwa mji wa Kyiv uko chini ya mashambulizi ya Urusi na akawahimiza wakaazi kutafuta maeneo salama ya kujihifadhi.

Mkuu wa utawala wa kijeshi wa Kyiv, Tymur Tkachenko, ametoa agizo kwa vikosi vya dharura kutumwa haraka katika maeneo yaliyoathirika ili kushughulikia athari za mashambulizi hayo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW