1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ligi ya Mabingwa: Real Madrid yaipiga Atletico katika debi

5 Machi 2025

Real Madrid iliendeleza ubabe wake wa debi ya Madrid kwenye jukwaa kubwa kabisa la Ulaya. Real waliwafunga wapinzani wao wakali Atletico mabao 2 - 1 mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 za mwisho ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Real Madrid
Real Madrid iliendeleza ubabe wake wa debi ya Madrid kwenye jukwaa kubwa kabisa la UlayaPicha: PIERRE-PHILIPPE MARCOU/AFP

Atletico ilipoteza fainali zake mbili kwa Real Madrid katika mwaka wa 2014 na 2016 na ikaondolewa mara mbili nyingine walipokutana katika duru ya mtoano -- katika robo fainali ya 2015 na nusu fainali ya 2017. Pia Jumanne, Arsenal ilipiga hatua kubwa kuelekea robo fainali baada ya ushindi wa 7 - 1 ugenini dhidi ya PSV Eindhoven. 

Katika usiku mzuri kwa vilabu vya Ligi ya Premier ya England, Aston Villa ilishinda 3 - 1 dhidi ya Club Brugge, na Borussia Dortmund ya Ujerumani ikatoka sare ya 1 - 1 na Lille ya Ufaransa. Hii leo, Paris Saint-Germain itaialika Liverpool, Inter Milan itakuwa ugenini kwa Feyenoord, Benfica itachuwana na Barcelona, na Bayern Munich itawakaribisha Wajerumani wenzao Bayer Leverkusen.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW