LISBON: Kadi Buluu kuvutia wataalamu wajuzi
13 Septemba 2007Matangazo
Kamishna wa sheria wa Umoja wa Ulaya,Franco Frattini amesema mwezi ujao atazindua “Kadi Buluu ya Leba“ ya Umoja wa Ulaya.Alipozungumza mjini Lisbon nchini Ureno kwenye mkutano uliohusika na masuala ya uhamiaji,Frattini alisema,pendekezo hilo litawasilishwa kwa wanachama 27 wa Umoja wa Ulaya tarehe 23 Oktoba.
Azma ya mradi huo ni kuwavutia Ulaya,wataalamu wenye ujuzi ambao wanatafuta ajira.Kadi Buluu itawapa wafanyakazi wenye ujuzi mkubwa,haki mbali mbali kuhusu usalama wa kijamii na hali za kufanya kazi katika nchi za Umoja wa Ulaya.