1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON Mataifa tajiri yakosolewa kwa uuzaji silaha

22 Juni 2005

Mataifa tajiri duniani yamelaumiwa na muungano wa kupigania haki za binadamu, kwa kuendeleza biashara ya uuzaji wa silaha, kwa serikali zinazozitumia silaha hizo kufanya vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu.

Muungano huo, unaoyajumulisha mashirika ya Oxfam na Amnesty International, unasema mataifa yaliyoelendea zaidi kiviwanda duniani, G8, ikiwemo Ujerumani, yanatakiwa kuchukua dhamana kwa asilimia 80 ya silaha zinazouzwa ulimwenguni kote. Kiasi kikubwa cha silaha hizi huuziwa mataifa maskini zaidi na ambayo yameelezewa kuongoza katika ufisadi na ulaji rushwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW