1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Louise Arbour kuwa Mjumbe wa Haki za Binadamu wa UM

21 Februari 2004
NEW YORK: Mwanasheria wa Kikanada Bibi Louise Arbour ameteuliwa kuwa Mjumbe Maalumu Mpya wa Haki za Binadamu wa UM. Mjini New York, Katibu Mkuu Kofi Annan alitangaza kuteuliwa rasmi kwa Bibi Arbour mwenye miaka 57. Bibi Arbour aliyekuwa Mtoa Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya UM ya Kuhukumu Wahalifu wa Kivita mjini The Hague, Uholanzi, atakuwa mfuasi wa Sergio Vieira de Mello, aliyeuawa hapo mwaka jana makao makuu ya UM mjini Baghdad yaliposhambuliwa kwa bomu. Mashirika ya Kimataifa ya Haki za Binadamu yamekaribisha kuteuliwa kwa Bibi Arbour ambaye kuteuliwa kwake kutabidi kuidhinishwa na Hadhara Kuu ya UM.
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW