1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBrazil

Rasimu ya kwanza ya makubaliano ya Cop30 inawasilishwa

19 Novemba 2025

Mwenyeji wa mkutano wa COP30, Brazil imewasilisha rasimu ya kwanza ya makubaliano baada ya mazungumzo ya kimazingira ya Umoja wa Mataifa kuendelea hadi usiku,

Brazili Belem 2025 | Rais wa Brazili Lula da Silva katika ufunguzi wa mkutano wa hali ya hewa wa COP30
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva akitoa hotuba wakati wa sherehe ya ufunguzi wa Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Umoja wa Mataifa wa COP30 huko Belem, Para State, Brazil mnamo Novemba 10, 2025.Picha: Pablo Porciuncula/AFP

Rasimu hiyo iliwasilishwa wakati Rais Luiz Inácio Lula da Silvaalipotangaza kuwa anarudi Belem, jiji lililo ndani ya msitu wa mvua ambako mazungumzo yanaendelea, katika juhudi za kufanikisha makubaliano.Rasimu hiyo inatoa wigo wa matokeo yanayowezekana, ikionyesha tofauti kubwa kati ya takriban mataifa 200 yanayoshiriki mkutano huo katika Amazon, na safari iliyosalia kufikia makubaliano ya mwisho.Hati hiyo yenye kurasa tisa inashughulikia maeneo makuu yenye mvutano huko Belem: hatua za kibiashara, madai ya ufadhili zaidi kwa mataifa maskini, na upungufu wa ahadi za kitaifa za kupunguza hewa ya ukaa.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW