1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Lumbala atangaza mgomo wa kula kupinga kesi dhidi yake

15 Novemba 2025

Aliyekuwa kiongozi wa waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Roger Lumbala, ameanza mgomo wa kula ili kupinga kesi dhidi yake iliyoanza wiki hii .

Roger Lumbala
Aliyekuwa kiongozi wa waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Roger Lumbala (kushoto) asaini nyaraka kabla ya mkutano na waandishi wa habari Kampala Februari 6, 2013Picha: Isaac Kasamani/AFP/Getty Images

Lumbala, ambaye aliwafukuza mawakili wake na kukataa kufika mahakamani baada ya siku ya kwanza ya kesi Jumatano akidai kuwa mahakama hiyo ya Ufaransa haina uhalali wa kumshtaki, alitangaza mgomo wake wa kula katika taarifa iliyosomwa na mkuu wa mahakama ya jinai ya Paris, Marc Sommerer.

Hata hivyo Daniele Perissi, mkuu wa mpango wa Kongo katika shirika lisilo la kiserikali TRIAL International, moja ya makundi yanayowakilisha asasi za kiraia, ameliambia shirika la habari la AP kwamba mbinu za Lumbala zinalenga kuvuruga na ni juhudi za kuepuka uwajibikaji. Ameitaka mahakama hiyo kuhakikisha kwamba haki iliyocheleweshwa haizuiwi kutekelezwa.  Wizara za sheria za Kongo na Ufaransa hazijatoa tamko kuhusu hali hiyo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW