1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

M23 wataka waliotoroka Uvira kurejea nyumbani

12 Desemba 2025

Msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka amewatolea mwito wakongomani walioutoroka mji wa kimkakati wa Uvira kurejea nyumbani. Wakaazi wengi huko wamekimbilia nchi jirani ya Burundi.

DR Kongo Uvira 2025 | M23-Rebellen rücken auf die Grenzstadt Uvira vor
Picha: AFP

Msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka, ametoa wito kwa wakaazi hao kurejea nyumbani bila hofu yoyote.

Waasi hao wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda, wamethibitisha kuuteka kikamilifu mji huo wa kimkakati wa Uvira, Mashariki mwa Kongo, baada ya mapambano makali kati ya vikosi vyake na wanajeshi wa serikali. 

Mapambano hayo mapya yalianza tangu mwanzoni mwa mwezi huu huku Marekani ikijaribu kutuliza hali katika mgogoro huo.

Uvira ni mji muhimu wa kibandari Kaskazini mwa mto Tanganyika na uko karibu sana na mji wa kiuchumi wa Bujumbura nchini Burundi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW