MigogoroIsrael
Maafisa usalama wastaafu wa Israel waomba msaada wa Trump
4 Agosti 2025
Matangazo
Maafisa hao ambao ni pamoja na wakuu wa zamani wa mashirika ya intelijensia wamesema kwa tathmini yao ya kitaalamu, Gaza sio tishio tena kwa Israel.
Wamesema hayo kwenye barua ya wazi iliyotangazwa na vyombo va habari mapema leo, wakimuomba Trump kusimamia maamuzi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na hasa kuhusiana na usitishwaji mapigano.
Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Usalama la Israel Ami Ayalon ameonya kwamba vita hivyo vinavyokaribia mwezi wa 23 vinaifanya Israel kudhoofika kiusalama na kupoteza utambulisho wake.