1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maafisa wa Hawaii wazuia watalii kwenda kisiwa cha Maui

14 Agosti 2023

Maafisa katika Visiwa vya Hawaii wamewashauri watalii kutokwenda Maui wakati huu ambapo hoteli zitakuwa zikiwahifadhi watu wanaoondolewa kwenye kisiwa hicho, pamoja na vikosi vya msaada wa dharura.

Hawaii Lahaina | Zerstörung nach den Waldbränden auf Maui
Picha: Rick Bowmer/AP Photo/picture alliance

Mji wa kihistoria wa Maui umeharibiwa vibaya na moto mkubwa kabisa wa nyikani kuwahi kushuhudiwa ambao pia umesababisha vifo vya zaidi ya watu 90.Karibu wakaazi 46,000 pamoja na wageni wamekimbilia katika uwanja wa ndege wa Kahului ulioko Maui Magharibi, tangu kuibuka kwa janga hilo, hii ikiwa ni kulingana na Mamlaka ya Utalii ya Hawaii.Jana, wakazi wa Hawaii walifanya ibada maalumu kwa ajili ya wahanga wa moto huo, wakati wakijiandaa kuanzisha upya maisha. Gavana Josh Green amesema vyumba 500 vya hoteli vitatengwa kwa ajili ya wakazi wasio na makazi na vingine 500 kwa ajili ya wafanyakazi wa mamlaka ya masuala ya dharura ya shirikisho.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW