MigogoroAfrika
Maandamano baada ya uchaguzi yaendelea Tanzania
30 Oktoba 2025
Matangazo
Baadhi ya maeneo ya mji huo yaliyoshuhudia mwendelezo wa maandamano Alhamisi ni pamoja na Mbagala, Gongo la Mboto na Kiluvya kulingana na watu walioshuhudia.
Raia wa Tanzania waliianza kuingia barabarani jijini Dar es salaam na katika miji mingine kutokana na kile kinachotajwa kuwa ukandamizaji mkubwa dhidi ya upinzani na wakosoaji wa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Amri ya kutokutoka nje yatangazwa
Jana Jumatano, polisi nchini humo walitangaza marufuku ya kutokutoka nje kuanzia saa kumi na mbili jioni wakati ambapo huduma ya intaneti imezuiwa. Watumishi wa umma na wanafunzi wameamriwa pia kubaki nyumbani Alhamisi kutokana na ghasia zinazoendelea.