JamiiMadagascar
Maandamano ya vijana wa GenZ yaendelea kushuhudiwa Afrika
5 Oktoba 2025
Matangazo
Huko nchini Madagascar waandamanaji walimiminika jana katika mitaa ya mji mkuu Antananarivo wakimtaka rais Andry Rajoelina kujiuzulu, harakati ambazo rais huyo amezitaja kuwa jaribio la mapinduzi. Umoja wa Mataifa umesema hadi sasa watu 22 wameuawa huku mamia ya wengine wakijeruhiwa.
Nchini Morocco, vijana waliandamana kwa siku ya nane mfululizo hapo jana wakidai uwepo wa huduma bora za afya na elimu. Hivi majuzi maandamano hayo yaligeuka kuwa ya vurugu na kusababisha vifo vya watu wawili huko Agadir, kitendo kilichozidisha hasira ya waandamanaji katika taifa hilo la Kifalme.