Mabalozi wa NATO kukutana na wenzao wa Ghuba
11 Machi 2026
Matangazo
Mabalozi kutoka nchi 32 wanachama wa jumuiya ya kujihami ya NATO wanapanga kukutana na wawakilishi wa eneo la Ghuba wiki ijayo kujadili vita vya Iran na mvutano wa kikanda.
Hayo ni kwa mujibu wa wanadiplomasia watatu wa Ulaya walipozungumza na shirika la habari la Reuters.
Wanadiplomasia hao walisema mabalozi hao wanatarajiwa kufanya majadiliano na wenzao kutoka Bahrain, Kuwait, Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu.