1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaEcuador

Machafuko yasababisha vifo vya wafungwa 31 gerezani Ecuador

10 Novemba 2025

Wafungwa hao waligunduliwa wamekufa kwa kukosa hewa kwa sababu ya hali inayoashiria kujinyonga au kunyongwa.

Ecuador Machala 2025 | Polisi Ecuador karibu na gereza ambalo wafungwa 31 walifariki baada ya machafuko
Wafungwa wasiopungua 27 wamefariki gerezani nchini Ecuador katika mazingira ya kutatanisha.Picha: Luis Suarez/AFP

Wafungwa 31 mmoja wamefariki katika gereza moja nchini Ecuador.

Hayo yamesemwa na mamlaka ya gereza SNAI, na kueleza kuwa, wafungwa 27 waliokufa waligunduliwa Jumapili jioni.

Kulingana na maafisa hao, wafungwa hao walikufa kwa kukosa hewa kwa sababu ya kujinyonga au kunyongwa. Lakini haijabainika kikamilifu matukio yaliyosababisha vifo vyao.

Awali, mamlaka hiyo iliripoti kwamba wafungwa wanne waliuawa wakati wa machafuko ndani ya gereza hilo lililoko mji wa pwani ya Ecuador, Machala. Mamlaka hiyo imesema Idara husika zimeshaanza uchunguzi kuhusu kisa hicho.

Watu wengine 34 walijeruhiwa akiwemo afisa wa polisi wakati wa machafuko hayo.