1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Machar yuko tayari kujibu kesi inayomkabili

20 Septemba 2025

Makamu wa rais wa zamani wa Sudan Kusini Riek Machar yuko tayari kujibu kesi inayomkabili na atafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu. Haya ni kulingana na wakili wake Kur Lual Kur.

Sudan Kusini, Juba 2018 | Riek Machar
Makamu rais wa zamani wa Sudan Kusini, Riek MacharPicha: Bullen Chol/AP/dpa/picture alliance

Kur Lual Kur amesema mshtakiwa yuko tayari kwa kesi na pia kwamba yuko katika afya njema.

Alithibitisha kuwa Machar atahudhuria kikao hicho cha kwanza maalum cha mahakama siku ya Jumatatu kufuatia wito uliotolewa lakini akasema bado wanasubiri maelezo zaidi.

Upande wa utetezi umekanusha mashtaka dhidi yake yanayojumuisha mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu pamoja na madai kwamba aliagiza wapiganaji wa kikabila kushambulia kambi moja ya kijeshi mwaka huu na kusema ni sehemu ya juhudi za Rais Salva Kiir za kuutenga upinzani na kudumisha mamlaka.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW