1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron aanza ziara ya siku tano katika Bahari ya Hindi

Saleh Mwanamilongo
21 Aprili 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amewasili Mayotte Jumatatu, ikiwa ni kituo cha kwanza katika ziara yake ya siku tano katika maeneo ya Bahari ya Hindi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron awasili Mayotte kwa ziara ya kikazi
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron awasili Mayotte kwa ziara ya kikaziPicha: Marin Ludovic/abaca/picture alliance

Macron, akiambatana na mkewe Brigitte, atatumia siku moja kukutana na wakaazi na wabunge wa visiwa vya Mayotte na kuchukua tathmini ya ujenzi mpya wa visiwa hivyo, ambavyo bado vinakabiliwa na madhara ya Kimbunga Chido kilichopiga eneo hilo mnamo Desemba mwaka jana.

Rais Macron anawasili na rasimu ya sheria ya "kujenga upya" visiwa hivyo, ambayo inalenga pia kuimarisha vita dhidi ya uhamiaji haramu, makazi haramu, ukosefu wa usalama na kufufua uchumi wa ndani.

Baada ya visiwa vya Mayotte na Reunion, Macron atasafiri kwenda Madagascar na Mauritius kushughulikia mada za usalama wa baharini na ulinzi wa bahari, katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na uchafuzi wa plastiki.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW