1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Macron aitisha mkutano wa dharura kujadili Greenland na Iran

15 Januari 2026

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameitisha kikao cha dharura cha baraza la mawaziri la ulinzi mjini Paris kujadili dhamira ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kukiteka kisiwa kinachojitawala cha Greenland.

Zayed Military City 2025 | Emmanuel Macron awatembelea wanajeshi wa Ufaransa
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akihutubia wanajeshi wa Ufaransa wakati wa hafla moja katika kambi ya kijeshi ya Zayed karibu na Abu Dhbai mnamo Desemba 21, 2025Picha: Ludovic Marin/AFP

Afisa mmoja wa Ufaransa, amethibitisha kuwa mkutano huo ulikuwa umepangiwa kuanza saa mbili asubuhi kwa majira ya eneo hilo.

Katika chapisho la jana usiku kwenye mtandao wa X, Macron alisema kundi la kwanza la wanajeshi wa Ufaransa tayari linaelekea Greenland kushiriki katika zoezi la kijeshi lililoandaliwa na Denmark na Greenland.

Amesema kwa ombi la Denmark, aliamua kwamba Ufaransa itashiriki zoezi hilo la pamoja na kwamba kundi lingine litafuata baadaye.

Mataifa washirika yakiwemo Ujerumani, Norway na Sweden pia yameanza kupeleka wanajeshi wake Greenland kuonyesha mshikamano wao kwa Denmark na Greenland.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW