1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Macron asaini sheria tata ya pensheni

15 Aprili 2023

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesaini sheria ya kurefusha umri wa pensheni, kufuatia hatua ya Baraza la Katiba kuuidhinisha muswada wa sheria hiyo Ijumaa.

Frankreich Paris | Demonstration gegen Macrons Rentenreform | Feuerwehr, brennendes Auto
Picha: Ewen Bazin via REUTERS

Chini ya sheria hiyo inayopingwa vikali na vyama vya wafanyakazi, umri wa kustaafu na kupata malipo ya uzeeni utapandishwa kutoka miaka 62 hadi 64.

Baada ya kupitishwa kwa sheria hiyo yamezuuka maandamano makubwa na yenye vurugu katika miji mingi kote nchini Ufarnsa, ambapo watu 112 wameripotiwa kukamatwa na polisi mjini Paris pekee.

Waandamanaji wamezichoma moto baiskeli, skuta za umeme na mapipa ya taka katika mji huo mkuu, na katika mji wa Rennes, mlango wa kituo cha polisi na ofisi ya bunge vimeharibiwa katika ghasia hizo.

Awali vyama vya wafanyakazi vilikuwa vimemtaka Rais Emmanuel Macron kutoisaini sheria hiyo, na vimekataa mwaliko wake kwa mazungumzo Jumanne ijayo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW