Macron awasili Kenya kutokea Misri
11 Mei 2026
Matangazo
Hii ni kama sehemu ya ziara yake barani Afrika inayolenga kufufua mahusiano ya Ufaransa na bara hilo baada ya miaka kadhaa ya kuvurugika kwa mahusiano hayo.
Katika ziara hiyo Macron atahudhuria mkutano wa kilele wa siku mbili utakaoanza leo Jumatatu.
Mkutano huo utawaleta pamoja viongozi wa Afrika na wakurugenziwa kibiashara, mwaka mmoja kabla muhula wake kufikia mwisho.
Afisi ya Macron imesema mkutano huo wa kilele utajikita katika ustawi wa kiuchumi na uwekezaji miongoni mwa masuala mengine. Macron amewasili Kenya kutoka Misri na katika ziara hiyo anatarajiwa pia kuelekea Ethiopia.