1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Macron na Modi wafanya mazungumzo New Delhi

17 Februari 2026

Viongozi hao wamejadiliana kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kimkakati mjini New Delhi ambako Macron yuko ziarani

Rais Emmanuel Macron akiwa pamoja na waziri mkuu Narendra Modi
Rais Emmanuel Macron akiwa pamoja na waziri mkuu Narendra ModiPicha: Ludovic Marin/AFP/Getty Images

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amefanya mazungumzo na waziri mkuu wa India Narendra Modi yaliyolenga kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kimkakati, wakati mataifa hayo mawili yakitafuta ushirikiano wa karibu zaidi kufuatia hali ya mashaka inayoikabili dunia pamoja na kubadilika kwa mirengo ya siasa za kikanda.

Emmanuel Macron

Mazungungu hayo yamefanyika mjini New Delhi yakijikita zaidi katika kukuza ushirikiano kwenye masuala ya ulinzi, biashara, teknolojia na nishati huku Ufaransa ikijinadi kama mmoja wa washirika muhimu wa kutegemewa na India barani Ulaya.

Viongozi hao wawili pia wamezinduwa kwa pamoja kiwanda cha kukamilisha uundaji wa helikopta chapa H125 katika jimbo la Karnataka Kusini mwa India.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW