Macron: Ulinzi wa kujitegemea Ulaya haufai
13 Julai 2026
Matangazo
Kauli hiyo inajiri wakati serikali za mataifa hayo zikiongeza bajeti zao za kijeshi kutokana na kitisho cha Urusi na shinikizo la Marekani kutaka nchi hizo kuongeza bajeti zao za ulinzi.
Hotuba ya Macron katika ufunguzi wa mkutano wa washirika wa Ukraine unaojulikana kama "muungano wa walio tayari" unaofanyika mjini Paris, imekuja mwezi mmoja baada ya kuvunjika kwa mradi wa pamoja wa Ufaransa na Ujerumani wa kutengeneza ndege za kivita kufuatia miezi kadhaa ya mkwamo kati ya kampuni za ulinzi.
Hali hiyo imeonyesha ushindani wa kiviwanda unaoweza kudhoofisha juhudi za Ulaya za kujiimarisha kijeshi.