1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maduro ataka 'mkono wa chuma' wa serikali kuzima maandamano

13 Agosti 2024

Rais Nichola Maduro amewalaumu viongozi wa upinzani, Edmundo Gonzalezi Urrutia, na Maria Corina Machado kwa kuchochea machafuko nchini Venezuela, na kuzitaka taasisi za kutumia kutumia "mkono wa chuma."

Venezuela l Rais Nicholas Maduro
Rais Maduro ameagiza nguvu ya ziada itumike kuzima maandamano ya wapinzaniPicha: Matias Delacroix/AP/dpa/picture alliance

Rais wa Venezuela Nicholas Maduro ametoa wito kwa taifa kutumia kile alichokiita "mkono wa chuma" baada ya maandamano mabaya kupinga kuchaguliwa kwake tena mwezi Julai, kulikotajwa ndani na nje kama kichekesho.

Wakati idadi rasmi ya vifo vya maandamano hayo ikipanda hadi 25, Maduro amehimiza sheria kali kwa vurugu alizolaumu kwa upinzani, ambao unasisitiza kuwa mgombea wake Edmundo Gonzalezi Urrutia alishinda uchaguzi wa Julai 28 kwa kishindo.

Polisi wenye pikipiki wakiwa mbele ya kituo cha mabasi katika kitongoji chenye watu wengi cha Petare mjini Caracas mnamo Agosti 5, 2024.Picha: YURI CORTEZ/AFP/Getty Images

Soma pia: Upinzani Venezuela waitisha maandamano ya dunia Agosti 17

Maandamano makubwa yalizuka baada ya Maduro kutangazwa rais mteule na tume ya uchaguzi, ambayo inatazamwa kama tiifu kwa utawala wake. Waangalizi wameripoti ukandamizaji mbaya wa vikosi vya usalama, ambapo zaidi ya watu 2,000 wamekamatwa.

Maduro anawalaumu Gonzalez Urrutia na kiongozi maarufu wa upinzani Maria Corina Machado, ambaye alizuwiwa kugombea urais na taasisi zinazoegemea serikali.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW