Maelfu bila nguvu za umeme baada ya mashambulizi Urusi
25 Machi 2026
Matangazo
Haya ni kwa mujibu wa gavana wa eneo hilo,Vyacheslav Gladkov.
Gladkov amesema huduma za kupasha joto na majizimeathirika kwa wakaazi wengi pia huku nyuzi joto katika eneo la Belgorod zikitarajiwa kuwa chini ya sifuri katika siku chache zijazo.
Haya yanafanyika wakati ambapo mashambulizi ya Urusi nayo yamesababisha uharibifu katika vituo viwili vya nishati katika eneo la kaskazini mwa Ukraine la Chernihiv.
Kulingana na kampuni ya usambazaji umeme eneo hilo, mashambulizi hayo yamesababisha zaidi ya watu laki mbili kuachwa bila huduma hizo.
Jeshi la Ukraine linasema Urusi imeshambulia kwa droni 147 usiku kucha ambapo 121 kati ya droni hizo zilidunguliwa.