1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maelfu waandamana Tigray dhidi vikosi vya kigeni

23 Mei 2023

Maelfu ya watu wameandamana katika mkoa wa kaskazini mwa Ethiopia wa Tigray wakidai kuondolewa kwa vikosi vya kigeni nchini humo.

Äthiopien Konflikt mit Tigray
Picha: AMANUEL SILESHI/AFP/Getty Images

Waandamanaji hao walioshuhudiwa katika miji mikubwa kama Mekele, Adigrat na Shire wameamuru pia kurejeshwa makwao kwa mamilioni ya watu waliolazimika kuondoka kufuatia mzozo wa jimbo la Tigray uliosababisha pia maelfu ya vifo.

Soma pia: Jeshi la kikanda lajiondoa mji wa kimkati wa Shire-Tigray

Kulingana na wafanyakazi wa mashirika ya kibinaadamu, vikosi vya Eritrea bado vimesalia katika ardhi ya Ethiopia. Serikali mjini Addis Ababa imekataa kuzungumzia suala hilo.

Wanajeshi wa serikali ya Ethiopia na washirika wao kutoka nchi jirani ya Eritrea na wale wa mkoa wa Amhara walipambana na vikosi vya Tigray kwa miaka miwili, na vita hivyo vilihitimishwa kwa makubaliano yaliyofikiwa mwezi Novemba mwaka jana.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW