1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mafuriko Indonesia, Sri Lanka: idadi ya vifo yafika 1,000

1 Desemba 2025

Idadi ya watu ambao wameuawa kwenye mafuriko mabaya ambayo yamekumba maeneo ya bara Asia imefika 1,000 siku ya Jumatatu.

Indonesia Padang Pariaman 2025 | Utafutaji wa waathiriwa baada ya mafuriko mabaya
Wakazi na waokoaji wanatafuta waathiriwa baada ya mafuriko na maporomoko ya ardhi kukumba Wilaya ya Padang Pariaman, Sumatra Magharibi, Indonesia, Novemba 29, 2025. Jumla ya watu 303 wamefariki na 279 bado hawajapatikana baada ya mafuriko ya ghafla na maporomoko ya ardhi kuathiri majimbo matatu katika eneo la Sumatra, kwa mujibu wa Shirika la Kitaifa la Usimamizi wa Maafa.Picha: Andri Mardiansyah/Xinhua/picture alliance

Maeneo ya baraAsia yanakumbwa na mafuriko mabaya ambayo yamesababisha maafa makubwa ikiwemo vifo.

Sri Lanka na Indonesia ndizo nchi ambazo zimeathiriwa zaidi, na zimepeleka wanajeshi kuwasaidia manusura.

Mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa iliyonyesha kwa muda mrefu wiki iliyopita kote katika kisiwa cha Sri Lanka na katika maeneo mengi ya kusini mwa Thailand na kaskazini mwa Malaysia.

Idadi hiyo ya vifo ndiyo maafa makubwa zaidi kutokea nchini Indonesia ambayo yamesababishwa na majanga ya asili, tangu janga la Tetemeko la ardhi lililosababisha Tsunami na kuuwa zaidi ya watu 2,000.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW