1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Magazetini: Papa Francis; Utoaji mimba ni sawa na kuuwa

Sekione Kitojo
11 Oktoba 2018

Wahariri wa magazeti ya hapa Ujerumani wamejishughulisha zaidi leo(11.10.18 na uchaguzi katika  jimbo la Bavaria Jumapili ijayo, matamshi ya kiongozi wa kanisa Katoliki kuhusu utoaji mimba,na mfumko wa bei nchini Uturuki

Vatikan Papst Franziskus während der Generalaudienz
Picha: picture-alliance/NurPhoto/M. Valicchia

 

Mhariri wa  gazeti  la  Mittelbayerische Zeitung la  mjini Regensburg  akizungumzia  kuhusu  uchaguzi  wa  jimbo la  Bavaria , anaandika  kwamba , kitu kinachoshangaza  ni kwamba  chama  cha  CSU kinachoongoza  jimbo hilo hakijielekezi  kuiangalia  kwa makini  siku  ya  uchaguzi, kuweza kujipanga  kupata wingi  wa  kutosha  kuweza kushikilia  uongozi  wa  jimbo hilo, badala  yake viongozi wanalumbana  na  kutupiana  lawama , hususan mwenyekiti wa  chama  hicho  na  waziri wa mambo ya ndani Horst Seehofer  kuwa  ndiye anayesababisha  chama hicho  kushindwa. Mhariri  anaandika.

 

Kutokana  na malumbano juu  ya ilani ya  sera  ya uchaguzi  ya  chama  hicho , suluhisho bila  shaka  liko wazi. Tatizo  la  chama  cha  CSU  limefika  mbali  zaidi. Hata  suala  kumhusu  katibu  mkuu  wa  chama  Markus Soeder, linapaswa  katika  muktadha  huu kuulizwa, hata kama anauungwaji mkono  mkubwa  ndani  ya  chama hicho. Kwa nini mgombea mkuu  katika  uchaguzi awe hahusiki  katika  matokeo ya  uchaguzi ?

 

Mhariri  wa  gazeti la  Rhein-Zeitung  la  mjini  Koblenz  akiandika kuhusiana  na  uchaguzi  huo  wa  jimbo  la  Bavaria anasema:

 

Siku  ya  Jumapili  itakuwa  tu  mwanzo  wa  wa chama  cha  CSU kukaribia kupoteza ,  mamlaka  yake  katika  jimbo  hilo. Na  pia  ni hatua  ya  kufikia  mwisho kwa  shughuli  za  kisiasa  za  baadhi  ya viongozi. Uchaguzi  wa jimbo hilo  ambalo kimsingi lilikuwa linaongozwa na chama hicho, hautaamuliwa  na  kingine  isipokuwa uongozi wa  kiimla na siasa za kijinga.

 

Baada ya  kiongozi  wa  kanisa  Katoliki kusema  kwamba  utoaji mimba  ni  sawa  na  kumlipa  mtu kufanya  mauaji, gazeti  la Badische Zeitung  la  mjini  Freiburg limemkosoa sana  kiongozi huyo  wa  kidini  kwa  kuandika:

 

Ni  nini  alichokuwa  akilenga  kiongozi  huyo  mkuu  wa  kanisa Katoliki  kwa  matamshi  kama  hayo  na  alikuwa  akiwalenga  watu gani ? Bila  shaka  sio wanawake  ambao  wanajiweza  ambao wanaamua  kwamba  hawataki  watoto. Pia  si  binadamu , ambao wanataka  kuwasaidia  wanawake  ambao  wako  katika  hatari  ya kupoteza  maisha. Papa  anawaweka  wanawake  hawa  katika  hali ya  unyanyapaa, na  kama  kiongozi  mkuu  wa kanisa  Katoliki hatambui  kwamba amewaweka  katika  hali  ngumu  ya  kimaisha wanawake  hawa.  Hata  katika  uongozi  wa  papa  Francis , kanisa limejitenga, na  kujijengea  ukuta.

 

Nalo  gazeti  la  Allgemeine Zeitung la  mjini  Mainz likizungumzia matamshi  hayo  ya  papa  Francis , limeandika:

 

Papa huwa hakosei.  Lakini  hapa  sio  tu  kwamba  Papa  amefanya makosa  makubwa, lakini  kuna  mengi  zaidi: Amejitwika mzigo mkubwa  sana. Amefanya  madhambi. Kufananisha  utoaji  wa mimba  na  kumlipa mtu  kufanya  mauaji,  amekwenda  mbali  mno. Ni udhalilishaji  wa  hali  ya  juu, kusababisha  mgogoro  mkubwa inapotokea  mtu  akiamua  kutoa  mimba.

 

Mada ya mwisho  ni  kuhusu mfumko wa bei , ama  ughali  wa maisha  nchini  Uturuki. Mhariri  wa gazeti  la  Stuttgarter Nachrichten anaandika:

 

Hatua  za  hivi  karibuni  zilizochukuliwa  na  serikali  ya  Uturuki kupambana  na  ughali  wa  maisha  unaopindukia  mipaka  ni  ishara kwamba , serikali  ya  nchi  hiyo  inataka  kufanya  kila  inaloweza kuchukua  hatua  kali  zaidi. Kuwaweka  wakaguzi  wa  udhibiti  wa bei  kuchunguza bei katika  maduka ya  vyakula  nchini  humo  si mkakati  sahihi  wa  sera  za  kiuchumi. Serikali  ya  Erdogan inatapatapa  tu. Kwa  njia  hiyo haiwezi  kurejesha  imani  ya wawekezaji. Hata waungaji  wake  mkono  wanaanza  kulalamika. Erdogan  aliahidi  katika  kampeni  za  uchaguzi  kwamba  hali itaimarika, lakini  hadi  sasa  ni  mtafaruku  mtupu na  kupanda  kwa bei.

 

Hayo  ndio  machache  ambayo Sekione Kitojo  ameweza kutuchambulia  kutoka  kwa wahariri  wa  magazeti  ya  Ujerumani  hii leo.

Mwandishi: Sekione  Kitojo / inlandspresse

Mhariri:Yusuf Saumu

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW