Mahakama ya Kongo yauthibitisha ushindi wa Sassou N’Guesso
29 Machi 2026
Matangazo
Rais wa mahakama hiyo, Auguste Iloki, alitangaza uamuzi huo baada ya kukataa rufaa ya mgombea wa upinzani Uphrem Mafoula aliyekuwa akipinga matokeo ya uchaguzi.
Matokeo ya awali yaliyotolewa Machi 17 yalionyesha tayari kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 82 alikuwa anaongoza kwa mbali dhidi ya wagombea sita.
Vyama vikuu vya upinzani vilisusia uchaguzi huo, vikidai kuwa haukuwa wa haki, huku Rais Sassou-N'Guesso akiwa mgombea pekee aliyefanya kampeni kote nchini.
Kiongozi huyo ni miongoni mwa marais waliodumu madarakani kwa muda mrefu barani Afrika.
Hata hivyo, Kongo-Brazzaville inakabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi, zikiwemo deni kubwa, ukosefu wa ajira kwa vijana na umaskini uliokithiri.