1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

AfCHPR yatimiza miaka 20 tangu ilipoanza kazi zake Afrika

Veronica Natalis
13 Machi 2026

Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu na watu (AfCHPR) iliyopo Arusha Tanzania, imetimiza miaka 20 tangu ilipoanza rasmi kazi zake barani Afrika.

Tansania Arusha 2026 | Miaka 20 ya Mahakama ya Africa ya Haki za binadamu na watu.
Maadhimisho ya miaka 20 ya Mahakama ya Africa ya Haki za binadamu na watu, yaliyofanyika Arusha Tanzania.  Picha: The African Court on Human and Peoples' Rights (AfCHPR) Press Service

Hata hivyo miongoni mwa changamoto zinazoikabili mahakama hiyo ni utekelezaji wa maamuzi yake, pamoja na baadhi ya nchi wanachama kutoridhia au kujiondoa katika itifaki inayowaruhusu wananchi wao kupeleka kesi moja kwa moja katika Mahakama hiyo.

Ni katika kipindi ambacho pia Mahakama hiyo imempata Rais mpya aliyechaguliwa na majaji 11 wa Mahakama hiyo inayoshughulikia haki za binadamu, ikiwa ni uchaguzi wa kawaida wa kupokezana miongoni mwa majaji, nafasi inayodumu kwa kipindi cha miaka miwili.

Rais mpya wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu na watu kwa sasa ni jaji Braise Tchikaya raia wa Jamhuri ya Kidekokrasia ya Kongo, akichukua nafasi ya jaji Modibo Sako wa nchini Mali. Tchikaya anakabiliwa na kibarua cha kusimamia Haki za binadamu barani Afrika, hasa utekelezaji wa maamuzi ya Mahakama. Baada ya kuchaguliwa anasisitiza kuwa Mahakama hiyo inanguvu ya kupiga marufuku maamuzi binafsi ya mahakama za ndani.

Jaji Blaise Tchikaya raia wa DRC ambaye kwa Sasa ndio Rais wa Mahakama ya Africa ya Haki za binadamu na watu. Picha: The African Court on Human and Peoples' Rights (AfCHPR) Press Service

"Mahakama hii ni jukwaa la juu la kimataifa, maamuzi yote ya Mahakama za ndani za nchi binafsi na majaji 11 wa mahakama hii wananguvu ya kupiga marufuku maamuzi ya mahakama za ndani. Wakati Mahakama ilipoanzishwa baadhi ya maraisi walisema hakuna rasilimali za kutosha, lakini nchi kama Burkina Faso na Senegal zilisisitiza kwamba Mahakama ya Afrika inahitajika.”

Tanzania yatakiwa kurekebisha vifungu vyake vya katiba

Kesi za mwanzo zilizotolewa maamuzi ndani ya mwezi huu wa Machi chini ya Uongozi wa Tchikaya ni kuhusu uchaguzi na demokrasia ya Tanzania, ambapo mahakama hiyo imeipa Tanzania miezi 24 kurekebisha baadhi ya vifungu vyake katiba ya Tanzania bara na visiwani vinavyozuia mahakama za ndani kushughulikia pingamizi za matokeo ya uchaguzi wa urais.

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na makamu wake wa rais Dr Emmanuel Nchimbi.Picha: Courtesy of State House

Katiba ya Tanzania, inaruhusu Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC na katiba ya Zanzibar inaruhusu Tume ya Taifa ya uchaguzi Zanzibar ZEC kutokuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa matokeo ya uchaguzi yatahojiwa. Lakini huu sio uamuzi wa kanza wa Mahakama hiyo kwa Tanzania. Uamuzi wa sasa utakuwa na tofauti gani? Fulgence Massawe ni wakali aliyebobea katika masuala ya haki za binadamu.

"Kuna mabadiliko kidogo ya kanuni za Mahakama, kama utasikia amri nyingi zilizotolewa, mwishoni wanaipa Tanzania muda wa kuleta taarifa ya utekelezaji wa maamuzi. Huko nyuma maamuzi yalikuwa yanatolewa lakini inaachiwa nchi yenyewe ikatekeleze maamuzi inavyotaka, lakini kwa sasa kuna mfumo unayoipa mahakama mamlaka ya kuita nchi ili itoe taarifa kwa namna gani wametekeleza kwahiyo ni suala ya muda.”

Mahakama hiyo ya haki za Binadamu inayo mamlaka kisheria ya kupinga maamuzi ya Mahakama za ndani na kutoa uamuzi wa juu unaozingatia viwango vya haki za binadamu barani Afrika.

Marufuku kuripoti ushuhuda wa waathiriwa wa ghasia Tanzania

03:31

This browser does not support the video element.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW