1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya ICC yasema Rais Kibaki wa Kenya alikutana na Kundi la Mungiki

26 Januari 2012

Mahakama ya ICC imeshawishika kuwa Rais Mwai Kibaki alikutana na kundi la Mungiki kupanga machafuko ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

People are forced to demolish their homes during fighting between police and the Mungiki sect , Thursday, June 7, 2007 in the Mathare slum in Nairobi, Kenya. Gun battles erupted in a Nairobi slum Thursday, killing at least 10 people, as police conducted house-to-house searches for members of an outlawed sect accused of terrorizing Kenyans and leaving behind a string of beheaded corpses. An Associated Press reporter saw 10 corpses in the Mathare shantytown, considered a stronghold for the Mungiki sect. Police sealed off the slum and rounded up more than 100 people, ordering them to kneel on the ground as gunshots whizzed by. (AP Photo/Karel Prinsloo)
Mapigano kati ya kundi haramu la Mungiki na Polisi mwaka 2007Picha: AP

Tuelekee nchini Kenya ambapo joto la kisiasa linazidi kuchemka, sasa Mahakama ya Kimataifa ya jinai ICC imesema kwamba imeshawishika kuwa rais wa nchi hiyo, Mwai Kibaki, Naibu Waziri Mkuu Uhuru Kenyatta na Mkuu wa Utumishi wa Umma, Francis Muthaura, walikutana na kundi haramu la Mungiki tarehe 26 Novemba mwaka wa 2007 kupanga machafuko ya ghasia za baada ya uchaguzi.

Uhuru Kenyatta na Francis Muthaura ni miongoni mwa watuhumiwa wanne waliopatikana na kesi ya kujibu na mahakama hiyo ya ICC kwa kupanga ghasia za baada ya uchaguzi ambapo watu zaidi ya 1000 waliuwawa na wengine wengi kuwachwa bila makao.

Amina Abubakar amezungumza na Cyprian Nyamwamu wakili nchini Kenya kujua kauli hii ya ICC juu ya Rais Kibaki kukutana na Mungiki inamuweka katika nafasi gani.

Mwandishi:Amina Abubakar 

Mhariri: Mohammed Khelef

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi

Gundua zaidi

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW