1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya Juu Nigeria yabatilisha muundo wa sarafu mpya

4 Machi 2023

Mahakama ya Juu ya Nigeria imesema muundo wa sarafu mpya ya nchi hiyo, Naira, uliotolewa na Benki Kuu ni batili na kwamba muundo wa sasa unapaswa kuendelea kutumika.

Nigeria Änderung der Wähung Naira
Picha: Ubale Musa/DW

Oktoba mwaka uliopita, serikali ilitangaza mpango wa kutengeneza noti mpya na ikawapa raia wake muda wa hadi mwishoni mwa mwezi Januari kubadilisha sarafu yao ya zamani.

Hata hivyo, Jaji Emmanuel Agim alisema taratibu zinazofaa hazikufuatwa na noti chache mpya ndiyo zilitolewa.

Soma zaidi: Nigeria yaweka kikomo cha utoaji pesa zilizopo benki

Benki Kuu ilisema utengenezaji wa sarafu mpya ungeathiri mfumuko wa bei, lakini majimbo 16 yaliupinga mpango huo mahakamani, yakisema hayakupewa muda wa kutosha kufanya mabadiliko.

Mahakama ya Juu iliamua kwamba noti za zamani zinapaswa kuzingatiwa katika zabuni halali hadi ifikapo mwishoni mwa mwaka 2023.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW