1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama Ujerumani yakosoa mageuzi ya sheria ya uchaguzi

Josephat Charo
30 Julai 2024

Mahakama ya katiba ya shirikisho la Ujerumani imepitisha hukumu leo ikisema mageuzi ya sheria za uchaguzi zinazonuiwa kuuwekea mpaka ukubwa wa bunge kwa sehemu ni kinyume na katiba.

Picha ya Mahakama ya Kikatiba ya Shirikisho
Picha za Mahakama ya Kikatiba ya Shirikisho huko Karlsruhe Rhineland-Palatino Ujerumani .Picha: IMAGO/Political-Moments

Mageuzi hayo, yaliyopendekezwa na serikali ya mseto ya kansela Olaf Scholz, yanalenga kupunguza ukubwa wa bunge la Ujerumani Bundestag liwe na viti 630. Idadi ya sasa ya wabunge katika bunge hilo ni 733 kutokana na mfumo wa upigaji kura unaowapa viti washindi wa kura za maeneo ya uwakilishi, pamoja na viti vinavyopewa kila chama kulingana na idadi ya kura vilizoshinda kitaifa.

Chama cha kihafidhina cha Christian Social Union, CSU na chama cha mrengo mkali wa kushoto cha Die Linke vilikuwa vimewasilisha rufaa katika mahakama ya katiba mjini Karlsruhe kuhusu mageuzi hayo yaliyopitishwa na baraza la chini la bunge la Ujerumani mnamo Machi 2023. Vyama hivyo viliyapinga mageuzi hayo vikisema si ya haki kwao.

 

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW