1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya Uturuki yatoa waranti wa kukamtwa kwa Netanyahu

8 Novemba 2025

Mahakama moja ya Istanbul, Uturuki, imetoa waranti wa kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na maafisa wengine 36 wa serikali yake kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya ubinadamu na mauaji ya halaiki Gaza.

Israel Jerusalem 2025 | Netanyahu akiwa katika mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin NetanyahuPicha: Ohad Zwigenberg/AFP

Ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu wa Istanbul ilihalalisha hati hizo na kusema kwamba maafisa wa serikali ya Israeli wanapaswa kuwajibishwa kwa vitendo vya uhalifu dhidi ya ubinadamu na mauaji ya halaiki yaliyofanywa Gaza, pamoja na vitendo vilivyofanywa dhidi ya  msafara wa kupeleka misaada katika Ukanda wa Gaza.

Waendesha mashitaka wamesema kuwa, kutokana na uhalifu huo, maelfu ya watu, wakiwemo wanawake na watoto, walipoteza maisha, huku maelfu zaidi wakijeruhiwa na maeneo ya makazi yakiharibiwa.

Mara kwa mara,Israel imeshutumiwa kwa uhalifu wa kivita na, katika baadhi ya matukio, mauaji ya halaiki juu ya matendo yake katika Ukanda wa Gaza, shutuma ambazo imekanusha.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW