1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Abbas ahimiza kuondolewa vizingiti vya Israel kuhusu Gaza

14 Februari 2026

Kiongozi wa mamlaka ya wapalestina Mahmud Abbas ametoa wito wa kuondolewa vizingiti vyote alivyosema Israel imeviweka katika kutekeleza awamu ya pili ya usitishaji wa mapigano Gaza.

Deutschland Berlin 2022 | Treffen zwischen Mahmud Abbas und Olaf Scholz
Kiongozi wa mamlaka ya wapalestina Mahmud AbbasPicha: Sean Gallup/Getty Images

Akizungumza kwa niaba ya kiongozi huyo katika mkutano wa kilele wa 39 wa Umoja wa Afrika, Waziri Mkuu wa Palestina Mohammed Mustafa amesema kuondolewa kwa vizingiti hivyo kunahitajika ili kuhakikisha huduma muhimu zinaendelea kutolewa, kuratibu misaada ya kiutu na kuhakikisha waathirika wanapokea matibabu.

Abbas ameituhumu Israel kwa kuendelea kukiuka makubaliano kati yake na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas yaliyoanza kutekelezwa mwezi Oktoba mwaka jana na kuungwa mkono na Marekani.

Amesema tangu kutangazwa kwa makubaliano hayo zaidi ya wapalestina 500 wameendelea kuuawa katika Ukanda wa Gaza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika Mahmoud Ali Youssouf, wakati wa ugunzi wa mkutano huo wa siku mbili alisema mauaji ya watu wa Palestina ni lazima yakomeshwe.

Amesema mapigano hayo na mateso kwa watu wa Gaza kunatoa changamoto kubwa katika dhamira ya bara hilo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW