Makadinali kutoka kote duniani wakutana Vatican
26 Juni 2026
Mkutano huo wa dharura wa makadinali ulianza asubuhi kwa kikao cha kwanza cha kazi, huku majadiliano yakitarajiwa kuendelea hadi kesho Jumamosi.
Kwa mujibu wa Vatican, ajenda za mkutano huo zinajumuisha hali ya dunia kwa ujumla, maendeleo katika teknolojia ya akili mnemba na hatua zinazofuata katika mchakato wa mageuzi ya Sinodi ya Dunia ya Kanisa Katoliki.
Mikutano ya aina hii ni nadra sana. Tofauti na mikutano ya kawaida ya makadinali ambayo inaweza kufanyika mara kadhaa kwa mwaka, mkutano maalumu wa dharura huwakutanisha si tu makadinali wanaoishi Roma, bali makadinali wote zaidi ya 240 kutoka kote duniani.
Mkutano wa makadinali unachukuliwa kuwa chombo muhimu zaidi cha ushauri kwa Papa katika uongozi na maamuzi yanayohusu kanisa Katoliki.