1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makubaliano ya Israel na Hamas hayatofanyika kabla ya Ijumaa

23 Novemba 2023

Mshauri wa Israel kuhusu usalama imeonesha hatua ya kuachiliwa huru mateka wanaoshikiliwa na Hamas, chini ya makubaliano ya muda ya kusitisha vita kati ya Israel na kundi hilo la wanamgambo, haitofanyika kabla ya Ijumaa.

Israel Palestinians
Wapalestina wameketi katika eneo ambalo limeshambuliwa na Israel mjini Khan YounisPicha: Mohammed Dahman/AP/picture alliance

Ripoti hiyo imeondowa matumaini ya jamaa za wanaoshikiliwa mateka, waliotarajia watu wao kuachiliwa leo Alhamisi. Jana Jumatano, Israel na kundi la Hamas  walikubaliana kusitisha vita Gaza, kwa siku nne kupisha misaada ya kibinadamu pamoja na kuachiliwa huru kwa mateka wasiopungua 50 wanaoshikiliwa na Hamas, kwa kubadilishana na Wapalestina kiasi 150 waliofungwa katika jela za Israel.

Soma pia:Papa Francis akutana na jamaa za waliotekwa na Hamas na wafungwa wa Palestina

Taarifa zinasema mapigano yameshuhudiwa yakiendelea leo, huku utekelezaji wa makubaliano ya usitishaji vita ukisogezwa hadi kesho Ijumaa. Moshi mzito umeripotiwa kutanda katika anga ya eneo la vita la Kaskazini mwa Gaza.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW