Migogoro
Makubaliano ya kisitisha vita Syria yarefushwa kwa siku 15
25 Januari 2026
Matangazo
Wizara ya Ulinzi ya Syria imesema uamuzi huo unakusudia kuwezesha mchakato wa kuwahamisha wanamgambo wenye itikadi kali wanaoshikiliwa kwenye magereza kaskazini mashariki mwa Syria na kuwapeleka Iraq.
Mchakato wa kuwahamisha waliofungwa kwenda Iraq waanza
Vikosi vya Marekani vimeshaanza kuwahamisha wanamgambo hao wanaodaiwa kuliunga mkono kundi linalojiita Dola la Kiislamu (IS). Katika wiki za karibuni, serikali ya Syria imekuwa ikipambana dhidi ya maeneo hayo yaliyokuwa yakidhibitiwa na wanamgambo wa Kikurdi na imefanikiwa kuyadhibiti kwa kiasi kikubwa.