1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSudan

Makundi ya Sudan yaanza mazungumzo ya serikali ya mpito

10 Januari 2023

Vyama vya siasa nchini Sudan jana vilianza mazungumzo kujaribu kufikia makubaliano ya kuunda serikali ya kiraia na kutatua masuala mengine yaliyokwama kwa zaidi ya mwaka mmoja baada ya mapinduzi ya kijeshi.

Sudan Khartoum | Abkommensunterzeichnung - Abdel Fattah al-Burhan
Picha: AFP via Getty Images

Akizungumza jana na waandishi habari, mwanasiasa Khalid Omer Yousif, alisema kuwa lengo la matokeo ya mkutano huo ni kuwakilisha msingi mpana wa Wasudan na kueleza maoni ya wadau.

Mwezi uliopita, vyama hivyo vilisaini mkataba na jeshi kuanzisha kipindi kipya cha mpito wa kisiasa kuelekea kwenye uchaguzi. Lakini waandamanaji waliyakosoa makubaliano hayo wakisema hayana uwakilishi na yaliacha masuala yenye utata kwa ajili ya mazungumzo zaidi. Mazungumzo yajayo yataangazia masuala yaliyoachwa kwenye mfumo wa makubaliano ikiwemo, kipindi cha haki cha mpito, mageuzi katika sekta ya usalama, mpango wa amani uliosainiwa mwaka 2020 na mivutano mashariki mwa Sudan.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW