1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Malawi yapokea fidia ya dola mil.11 za athari za ukame

20 Agosti 2024

Serikali ya Malawi imepokea fidia ya bima ya dola za Kimarekani milioni 11.2 kutokana za athari za ukame unaohusishwa na El-Nino.

Malawi | hali ya ukame
Maeneo mengi yamekabiliwa na hali mbaya ya hewa nchini Malawi kutokana na hali ya El Nino na kusababisha hata mavuno kuwa hafifuPicha: Ashley Cooper/Global Warming Images/picture alliance

Kitita hicho kimelipwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika baada ya nchi hiyo kutangaza ukame kuwa janga la taifa mapema mwaka huu.

Fedha hizo zitasaidia kutoa chakula kwa kaya zipatazo laki 235,000 katika mikoa iliyoathirika zaidi na ukame.

Aidha pia, Benki ya Maendeleo ya Afrika imesema zaidi ya kaya laki 100,000 zitanufaika na msaada wa malipo ya moja kwa moja.

Rais wa Malawi Lazarus Chakwera ameyataja malipo hayo kuwa ni njia ya kuokoa maisha ya watu wanaoishi katika mazingira magumu nchini Malawi.

Mvua zilizonyesha kati ya mwezi Novemba na Aprili zikiambatana na hali ya El Nino zimechangia mazao kushindwa kustawi katika eneo la kusini mwa Afrika.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW