1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMali

Mali yasitisha makubaliano ya amani ya 2015 na waasi

26 Januari 2024

Utawala wa kijeshi nchini Mali umetangaza kusitisha makubaliano muhimu ya amani ya mwaka 2015 yaliyotiwa saini na makundi ya Kaskazini yanayotaka kujitenga, kufuatia miezi kadhaa ya uhasama kati ya waasi hao na jeshi

Waasi wa Muungano wa Azawad wakutana katika jangwa nje ya Menaka mnamo Machi 14,2020
Waasi wa Muungano wa AzawadPicha: Souleymane Ag Anara/AFP

Katika taarifa iliyopeperushwa kupitia televisheni, msemaji wa serikali ya Mali Abdoulaye Maiga, amesema utawala wa kijeshi nchini humo umetaja kuweko kwa mabadiliko miongoni mwa makundi yaliotia saini makubaliano hayo ya amani lakini pia "vitendo vya uhasama" vya mpatanishi mkuu, Algeria.

Soma piaMapigano yazuka kati ya waasi wa Tuareg na jeshi la Mali

Maiga amesema serikali ya Mali imebainisha kutowezekana kabisa kutekelezwa kwa makubaliano hayo.

Waasi waliushtumu utawala wa kijeshi kwa kutoheshimu makubaliano

Mnamo Julai 2022, waasi hao wanaotaka kujitenga, walioungana chini ya uratibu wa Harakati za Azawad (CMA), tayari walikuwa wameushtumu utawala huo wa kijeshi kwa "kutotekeleza" makubaliano hayo.

Makubaliano hayo yaliosimamiwa na Algeria, yalitaka kujumuishwa kwawaasi wa zamani katika vikosi vya ulinzi vya Mali pamoja na uhuru zaidi katika maeneo ya nchi hiyo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW