Mandamano makubwa yafanyika katika mkutano wa COP30, Brazil
15 Novemba 2025
Matangazo
Katika maandamano hayo yaliyopewa jina'' Maandamano kwa ajili ya Hali ya Hewa," waandamanaji wanadai haki katika suala zima la hali ya hewa na ulinzi wa ardhi ya jamii za asili ambazo ziko hatarini kutokana na ukataji miti na uchimbaji haramu wa dhahabu.
Tofauti na wakati wa mikutano ya hali ya hewa iliyopita katika mataifa kama vile Azerbaijan, maandamano yameruhusiwa kufanyika nchini Brazil wakati mazungumzo yakiendelea.
Hapo jana, watu kadhaa wa jamii za asili na wanaharakati wengine wa hali ya hewa walifunga lango kuu la kuingilia mkutano huo kwa saa kadhaa.
Katika mkutano huo wa COP30, takriban nchi 200 bado zinajadili hadi mwisho wa wiki hii namna ya punguza ongezeko la joto duniani kwa haraka zaidi.