1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Mapigano ya makundi hasimu yaitikisa Tripoli

13 Mei 2025

Mapigano makali kati ya makundi ya wanamgambo waliojihami kwa silaha nzito yameutikisa mji mkuu wa Libya, leo na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 6.

Libya| Tripoli| Mivutano
Tangu kuanguka utawala wa Muammar Gaddafi mwaka 2011, Libya inakumbwa na mapigano ya kila wakati baina ya makundi hasimu ya wanamgambo.Picha: Hamza Turkia/Xinhua/picture alliance

Maafisa kadhaa wamearifu kuwa milio la risasi na milipuko ilisikika hadi mapema leo Asubuhi mjini Tripoli baada ya kuzuka jana usiku kufuatia kuuawa kwa kamanda mmoja mwenye nguvu anayeongoza kundi la wapiganaji wenye silaha.

Afisa mmoja wa serikali amesema Kamanda huyo Abdel-Ghani al-Kikli wa kundi la SSA aliuawa na kundi hasimu linalofahamika kwa jina la Brigedi 444.

Inaarifiwa makabiliano yalishuhudiwa zaidi kwenye kitongoji cha Abu Salim kusini mwa Tripoli. Wizara ya Afya imesema watu sita wameuawa na inafanya kazi kuzihamisha familia zilizokwama katikati ya mapigano.

Mapigano hayo yameilazimisha izara ya elimu kuzifunga shule zote leo Jumanne na masomo kwenye Chuo Kikuu cha Tripoli yamesimamishwa kwa muda usiojulikana.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW