1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano yaendelea Sudan

5 Mei 2023

Mashambulizi ya anga na milio ya risasi vimesikika leo Ijumaa kwenye mji mkuu wa Sudan, Khartoum, huku kukiwa hakuna dalili zozote za mapigano kupungua, licha ya kitisho cha Marekani kuweka vikwazo vipya.

Sudan | Kämpfe in Khartum
Picha: AFP/Getty Images

Mamia ya watu wameuawa katika mapigano yaliyodumu kwa takribani wiki tatu kati ya majenerali wawili wanaohasimiana.

Mapambano yameendelea siku moja baada ya Rais wa Marekani, Joe Biden, kutishia kuwawekea vikwazo wale wanaohusika katika kudhoofisha amani, usalama na utulivu wa Sudan.

Wakati huo huo, Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), limezitolea wito serikali mbalimbali kuwaruhusu raia wanaokimbia vita Sudan kuingia kwenye ardhi zao na kutowarudisha kwenye nchi hiyo.

Soma zaidi: Marekani yatishia vikwazo vipya nchini Sudan

Elizabeth Tan, Mkurugenzi wa Ulinzi wa Kimataifa wa UNHCR, amesema wanazishauri serikali kuwatowarejesha watu Sudan kwa sababu ya mzozo unaoendelea huko.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW