1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maporomoko ya ardhi yauwa takriban watu 64 Ethiopia

12 Machi 2026

Takriban watu 64 wamefariki dunia na wengine 125 hawajulikani walipo baada ya maporomoko ya ardhi kukumba wilaya tatu kusini mwa Ethiopia kufuatia wiki moja ya mvua kubwa.

Ethiopia | Gondar Kaskazini
Eneo la maporomoko ya ardhi la Gondar Kaskazini nchini Ethiopia mnamo Agosti 24, 2024Picha: North Gondar zone Disaster Prevention department

Manuqa, mkurugenzi wa idara ya kushughulikia majanga katika eneo hilo, amesema maporomoko hayo yalitokea katika eneo la Gamo na kuathiri wilaya ya Gacho Baba, Kamba na Bonke.

Manuqa amesema mtu mmoja alitolewa kwenye tope akiwa hai wakati wa shughuli ya uokoaji.

Mkuu wa mawasiliano wilayani Gacho Baba, Abebe Agena, amesema wengi wa waliokufa walipatikana wakiwa wamezikwa kwenye tope.

Idadi ya nyumba zilizoathirika bado haijabainika.

Rais wa jimbo la kusini mwa EthiopiaTilahun Kebede, ameelezea masikitiko yake juu ya maafa hayo na kuwataka wakazi kuhamia maeneo ya juu wakati mvua inaendelea kunyesha.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW