SiasaHaiti
Marekani na Kenya wasaini makubaliano ya ulinzi
26 Septemba 2023![Moja ya makundi ya uhalifu katika mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince linaloongozwa na aliyewahi kuwa afisa wa polisi Jimmy "Barbecue" Charizier(katikati). Mji huo unakabiliwa na machafuko ya makundi hayo yanayotaka serikali ijiuzulu.](https://static.dw.com/image/66903029_800.webp)
Matangazo
Haiti inapambana na machafuko yanaoyasababishwa na makundi ya uhalifu na hasa katika mji mkuu Port-au-Prince.
Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin amesaini makubaliano hayo na mwenzake wa Kenya Aden Duale katika mkutano uliofanyika Nairobi.
Makubaliano hayo ni yanaongoza uhusiano wa kiulinzi kwa miaka mitano ijayo wakati taifa hilo likiongeza harakati zake dhidi ya kundi la wanamgambo wa Al-Shabaab zikiongezeka.
Austin ameishukuru Kenya kwa kujitolea kuongoza ujumbe wa amani nchini Haiti na kusema kwa mara nyingine kwamba serikali ya Marekani itashirikiana na Bunge ili kupata dola milioni 100 za ufadhili ilizoahidi pembezoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.