1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani inamatumaini kuhusu azimio la UN Gaza

13 Novemba 2025

Marekani kupitia waziri wake wa mambo ya nchi za nje Marco Rubio, imesema inamatumaini kwamba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litakamilisha azimio kuhusu Gaza.

Israel 2025 | Marco Rubio
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani, Marco Rubio amesema nchi yake ina matumaini kuhusu azimio la UN kuhusu amani ya Gaza Picha: Fadel Senna/UPI Photo/IMAGO

Azimio hilo linaunga mkono hatua ya kupelekwa kwa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani.

Rubio amesisitiza kuwa hatua muhimu zinapigwa na muafaka utapatikana hivi karibuni.

Huku hayo yakijiri, Rais wa Israel Isaac Herzog, pamoja na maafisa waandamizi wa jeshi, wamelaani vitendo vya walowezi wa Kiyahudi dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu, wakitaka kukomeshwa mara moja vitendo hivyo vinavyoongezeka.

Herzog aliyaelezea mashambulizi hayo kama "ya kushangaza na "makubwa". Naye Marco Rubio amesema vurugu hizo zinaweza kuathiri mpango wa amani wa Gaza.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW