Marekani isiruhusu Dola kuporomoka zaidi
30 Novemba 2007Matangazo
Waziri wa Uchumi wa Ujerumani Michael Glos ametoa mwito kwa Marekani kuchukua hatua ya kuzuia thamani ya Dola kuporomoka zaidi.Amesema,mauzo ya nje ya nchi za Ulaya yanaathirika kutokana na viwango vya ubadilishaji wa fedha.Glos akaongezea kuwa Marekani isijaribu kusawazisha matatizo yake ya kiuchumi kwa kuiachilia thamani ya Dola kushuka zaidi.