Rais wa Marekani Donald Trump amesema Marekani iko tayari kufanya biashara na nchi nyingine chini ya uongozi wake. Akiwahutubia viongozi wa kisiasa na biashara katika Kongamano la Kiuchumi Duniani huko Davos, Uswisi, Trump amesema ustawi wa kiuchumi unaofanyika Marekani kutokana na ajenda yake ya "Marekani kwanza" unazinufaisha nchi nyengine duniani pia.