1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani, Korea Kusini zakanusha kuingia Korea Kaskazini

11 Julai 2023

Marekani na Korea Kusini zimetupilia mbali madai ya Korea Kaskazini ya kwamba ndege za kijasusi za Marekani zimekuwa zikikiuka anga lake na kuitaka Pyongyang kujiepusha na vitendo au matamshi yoyote yanayozidisha uadui.

Südkorea F-35 Kampfjets in Übungsflug
Picha: South Korean Defense Ministry/UPI Photo/IMAGO

Hayo yanajiri baada ya dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Yo Jong, ambaye pia ni mmoja wa maafisa wakuu wa sera za kigeni wa kaka yake, Kim Jong Un, kudai kuwa ndege za kivita za nchi hiyo zilipambana kuifurusha ndege ya Marekani.

Soma zaidi: Japan itaharibu kombora litakalorushwa na Korea Kaskazini

Mapema jana, Wizara ya Ulinzi ya Korea Kaskazini iliishutumu Marekani kwa kurusha mara kadhaa ndege za upelelezi na za kimkakati katika anga lake na kuonya kwamba ndege zitakazokiuka mamlaka yake zinaweza kudunguliwa.

Soma zaidi: Korea Kaskazini: Ushirika wa Korea Kusini na Marekani utachochea uhasama

Hata hivyo, Marekani imeitolea wito Korea Kaskazini kujiepusha na kile ilichokiita kuwa ni "harakati za kuchochea mvutano" na badala yake "ishiriki katika diplomasia iliyo thabiti."

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW